Main menu:
Shule ya Biblia
"Mkamate sana elimu, usimuache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako." - (Mithali 4:13);
Zingatia: Katika "Matendo 8:30-31", tunapata kujifunza habari za Towashi [mtu wa Kushi] aliyekiri mbele ya Filipo kutokuyaelewa aliyokuwa akisoma katika chuo cha nabii Isaya na kumsihi Filipo apande garini kumsaidia. Basi ikiwa utashidwa kuelewa baadhi ya masomo haya vizuri usisite kuwasiliana nasi kwa msaada wa ufafanuzi.
Karibu tujifunze pamoja neno la Mungu.
MAFUNZO YA AWALI YA BIBLIA
Ili kuweza kupata uelewa vizuri wa masomo ya Biblia yatakayofuata ni vema kupitia kitabu hiki ili kupata mtiririko na mpangilio mzima wa Biblia ambao utakupa uraisi wa kufuatilia na kuelewa vizuri masomo mengine.
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
MUNGU NA KITABU CHAKE
"Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamfuatao" (Waebrania 11:6)
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
UCHUNGUZI WA AGANO LA KALE
"Bwana akamwambia Musa, Andika maneno haya; kwa kuwa mimi nimefanya agano nawe, na pamoja na Israeli, kwa mujibu wa maneno haya" (Kutoka 34:27)
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
MATENDO YA MITUME
Kitabu hiki kinaitwa "Matendo ya Mitume" kwa sababu kinaeleza baadhi ya matendo ya baadhi ya Mitume wa Yesu. Kinaeleza hasa mambo machache waliofanya Petro na Paulo.
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
KANISA LA AGANO JIPYA
Yesu alisema, "......juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda" (Mathayo 16:18).
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
DIBAJI KWA AGANO JIPYA
"Angalia siku zinakuja, asema BWANA, nitakapofanya agano jipya na nyumba ya Israeli, na nyumba ya Yuda. Si kwa mfano wa agano lile nililofanya na baba zao, katika siku ile nilipowashika mkono, ili kuwatoa katika nchi ya Misri;......................". (Yeremia 31:31-32)
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
SHERIA NA INJILI
"Torati ni nini basi? Iliingizwa kwa sababu ya makosa, hata aje huyo mzao aliyepewa ile ahadi; iliamriwa kwa utumishi wa malaika kwa mkono wa mjumbe." (Wagalatia 4:19).
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
MAFUNDISHO YA MADHEHEBU
"Bali nyinyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo ya kwamba waliwaambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakifuata tamaa zao wenyewe za upotevu. Watu hao ndio waletao matengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho" (Yuda 1:17-19).
Maelezo Zaidi
______________________________________________________________________________________________________________
Zingatia: Masomo yaliyoainishwa hapo juu ni masomo machache kati ya mengi yanayoratibiwa na shule yetu ya Biblia. Masomo hutolewa kwa muda wa miaka miwili, bila ya malipo yeyote.
Kwa mafundisho zaidi tunawakaribisha katika shule yetu ya Biblia yenye walimu walio na uzoefu na uelewa mkubwa katika neno la Mungu.
Kwa melezo zaidi, tafadhali usisite kuwasiliana nasi kwa kutumia nafasi iliyopo hapo chini au kwa anwani zetu zilizo ainishwa katika vitabu vyetu.